*UTI Sugu, PID Sugu = USUGU WA VIMELEA DHIDI YA DAWA , Stop Usimeze Antibiotic Tena Kabla Hujasoma Ukweli Huuβ¦π*
Umeshawahi kujiuliza kwanini unapewa antibiotics leo, unapata nafuu kidogo, kisha baada ya muda kidogo tatizo linajirudia tena....?
Unatembea kutoka duka moja la dawa hadi jingine, kila dozi unayojaribu haina jibu la kudumuβ¦β οΈ
> *Hali hiyo si bahati mbaya,Β Ni USUGU WA VIMELEA DHIDI YA DAWA....π*
β Hali ambayo mwili wako unakuwa uwanja wa majaribio, na wadudu wanao ishinda dawa badala ya dawa kuwashinda wao..
*Kwa nini inatokea..?* π
Kwa sababu kila mara unatumia antibiotics bila mpangilio sahihi, bila vipimo na ushauri wa dakitari, bila kukamilisha dozi zako, Ndiyo mwanzo wa vimelea kuwa sugu....
Ni kama vile unawapa nafasi ya kwenda shule, kuhitimu na kupata degree ya usugu...β οΈ
*Matokeo yake ni nini.?* π
β³ Maambukizi yanayorudia rudia na kukataa dawa..
β³ Gharama kubwa ya matibabu kila siku...
β³ Hatari ya matatizo makubwa zaidi mwilini mwako...
Sio kila homa ni UTI, Sio kila maumivu ni PID, Na sio kila antibiotic unayoiona dukani inakuhusu..
Tiba siyo dawa pekee. Ni nidhamu, ushauri wa kitaalamu na uelewa sahihi....
*Kama una UTI sugu, au PID inayorudia rudia kila baada ya kutumia dawaβ¦*
Nakushauri fanya Culture and Sensitivity Test kabla ya kumeza antibiotic nyingine...STOP βοΈ
*Kwa nini.?* π
β³ Culture test inatafuta aina halisi ya kimelea (bakteria) kilichosababisha maambukizi....
β³ Sensitivity test inaonyesha dawa ipi inaua vimelea hivyo na zipi hazifanyi kazi...
*Faida zake.!* π
β³ Unaepuka kutumia dawa kwa kubahatisha...
β³ Unalinda mwili wako usije ukawa uwanja wa majaribio ya antibiotic...
β³ Unapunguza hatari ya vimelea kujenga usugu wa kudumu...
*NB:* Kabla hujaanza dozi ya antibiotic kwa UTI, PID, au maambukizi yoyote yanayo jirudia mara kwa mara..
Muombe daktari ufanye culture and sensitivity test , Ni gharama ndogo ikilinganishwa na madhara makubwa ya kutumia dawa zisizofaa..
Uko tayari kuendelea kucheza na mwili wako, au uta fundisha akili yako nidhamu ya tiba sahihi kabla vimelea havijapata Ushindi wa mwisho dhidi ya dawa...?